Friday, October 31, 2014

SUAREZ ALISTAHILI KUWEPO KATIKA ORODHA ZA BALLON D'OR - BARTRA.

BEKI wa kati ya klabu ya Barcelona Marc Bartra amesema ameshangazwa kwa kukosekana kwa Luis Suarez katika orodha ya kugombea tuzo za Ballon d’Or. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay alifunga mabao 31 katika mechi 33 akiwa na Liverpool msimu uliopita huku 12 kati hayo akiwa amefunga mwaka huu na kutoa pasi za kusaidia 11. Lakini pamoja na mafanikio hayo, Suarez anaonekana bado kuandamwa na mzimu wa kumng’ata Giorgio Chiellini wa Italia katika Kombe la Dunia nchini Brazil na kumfanya kufungiwa miezi minne adhabu ambayo aliimaliza wiki iliyopita. Bartra anaamini mshambuliaji huyo ambaye alitengeneza bao la Barcelona lililofungwa na Neymar katika mchezo wa El Clasico dhidi ya Madrid, alitakiwa kuwepo katika orodha hiyo. Akihojiwa beki huyo mwenye umri wa miaka 23 amesema maeshangazwa kwa Suarez kuachwa kwani anadhani alikuwa na mwaka wenye mafanikio.

No comments:

Post a Comment