Friday, October 31, 2014

TAJIRI LA CARDIFF LAWEKEZA TENA KATIKA SOKA MAREKANI.

MMILIKI wa klabu ya Cardiff City Vincent Tan na nguli wa zamani wa mpira wa kikapu wa Marekani Magic Johnson ni miongoni mwa kundi la wawekezaji ambao wamepewa klabu mpya ya soka katika Ligi Kuu ya Marekani-MLS ya Los Angeles FC. Kundi hilo la uwekezaji pia linamjumuisha mmiliki mwenza wa klabu ya Queens Park Rangers-QPR, Ruben Gnanalingam sambamba na mchezaji wa zamani wa soka la wanawake la nchi hiyo Mia Hamm. Timu hiyo mpya wa Los Angeles itasajiliwa rasmi MLS mwaka 2017 sambamba na timu nyingine kutoka Atlanta. Tan ambaye pia anamiliki timu ya TK Sarajevo ya Bosnia aliiambia BBC kuwa atakuwa mmiliki mwenye hisa nyingi zaidi katika klabu hiyo mpya.

No comments:

Post a Comment