Wednesday, October 29, 2014

URUSI YAZINDUA NEMBO YAO YA KOMBE LA DUNIA 2018.

NEMBO rasmi itakayotumika katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi imezinduliwa jana katika Kituo cha Anga cha Kimataifa. Nembo hiyo ambayo imepambwa na rangi ya nyekundu na bluu ambazo ni rangi ya bendera ya taifa hilo huku ikionyesha utajiri wa asili na historia yake ya mafanikio na ugunduzi. Picha za nembo hiyo pia iliwekwa katika ukumbi maarufu wa Bolshoi jijini Moscow. Urusi ilishinda haki za kuandaa michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kuzibwaga nchi za Uingereza, Hispania, Ureno, Uholanzi na Ubelgiji.

No comments:

Post a Comment