Friday, November 21, 2014

ARSENAL VS MAN UNITED: GIROUD FITI, WELBECK HATIHATI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Arsenal, Olivier Giroud yuko fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Manchester United kesho katika Uwanja wa Emirates baada ya kupona kupona majeruhi ya mguu wake uliovunjika. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 28 alikadiriwa kuweza kurejea uwanjani baada ya mwaka mpya kutokana na majeri hayo aliyopata Agosti mwaka huu lakini sasa anaonekana kuwa fiti kwa ajili ya kurejea. Nahodha wa klabu hiyo Mikel Arteta pia yuko fiti baada ya kupona majeruhi ya msuli lakini meneja wa timu hiyo Arsenal Wenger amesema mabeki wake Laurent Koscielny na Mathieu Debuchy bado hawako fiti. Wenger amesema mbali na hao lakini pia bado ataendelea kumkosa Theo Walcott katika mchezo wa kesho huku Danny Welbeck naye akiwa katika hatihati kutokana na kupata matatizo ya msuli akiwa katika majukumu ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment