Friday, November 21, 2014

CITY BADO INA NAFASI YA SKUHINDA TAJI LA LIGI KUU - PELLEGRINI.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini bado ana uhakika wa kutetea taji la Ligi Kuu pamoja na kupitwa kwa alama nane na vinara Chelsea. City ambao watakuwa wenyeji wa Swansea City kesho baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa kumalizika, wamefanikiwa kushinda mechi moja kati ya sita za mashindano yote walizocheza hivi karibuni. Kiwango cha timu hiyo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya pia imekuwa ya kusuasua huku wakiwa katika hatari ya kushindwa kuvuka hatua ya makundi. Hata hivyo Pellegrini bado amekuwa na imani na kikosi chake kufanya vyema katika ligi ya nyumbani na Ulaya msimu huu. Pellegrini amesema sasa sio wakati wa kuangalia yaliyotokea nyuma kwani bado kuna mechi nyingi za kucheza katika ligi na Ulaya. Kocha huyo aliongeza kuwa bado kuna mechi 27 hivyo kuna alama zaidi za kupigania hivyo wataona itakavyokuwa mpaka mwishoni mwa msimu.

No comments:

Post a Comment