Friday, November 21, 2014

UNITED KUMKOSA BLIND WIKI SITA.

KLABU ya Manchester United amedai kuwa majeraha ya goti ya kiungo Daley Blind yatamuweka nje ya uwanja kwa wiki kadhaa na sio miezi sita kama ilivyotangazwa. Meneja wa United, Louis van Gaal amesema kitakachofanyika kwanza ni nyota huyo kupumzika kwa muda wa siku 10 halafu ndiyo waangalie ukubwa wa tatizo lake. Klabu hiyo ilileta mkanganyiko baada ya kutuma ujumbe katika ukurasa wake mtandao wa kijamii wa twitter kuwa kiungo huyo atakuwa nje kwa miezi sita ujumbe ambao hata hivyo ulifutwa haraka baadae. Van Gaal amesema hawezi kutabiri ni muda gani haswa Blind anaweza kuwa nje ya uwanja kwani wanasubiria vipimo vya afya lakini hadhani kama inaweza kufikia miezi sita. Blind aliumia wakati akiitumikia timu yake ya taifa ya Uholanzi katika mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016 dhidi ya Latvia ambao walishinda kwa mabao 6-0.

No comments:

Post a Comment