Friday, November 21, 2014

MANCINI KUANZA NA AC MILAN KESHO.

MENEJA mpya wa klabu ya Inter Milan Roberto Mancini anakabiliwa na kibarua kigumu mwishoni mwa wiki hii wakati atakapoanza kibarua chake kwa kupambana na mahasimu wao AC Milan katika mchezo wa Serie A. Mancini alirejea tena kuinoa Inter wiki iliyopita baada ya kutimuliwa kwa Walter Mazzarri kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo katika mechi za hivi karibuni. Wakati akiinoa klabu hiyo kati ya mwaka 2004 na 2008, Mancini aliisaidia kushinda mataji matatu mfululizo ya Serie A, mawili ya Kombe la Italia na moja la Super Cup. Mbali na mchezo huo ambao utachezwa Jumapili, kesho kutakuwa na mchezo mwingine utakaozikutanisha Lazio na Juventus.

No comments:

Post a Comment