Friday, November 21, 2014

SHEFFIELD YAMCHOMOLEA MBAKAJI EVANS KUFANYA NAO MAZOEZI.

KLABU ya Sheffield United imesitisha ofa yake ya kumruhusu Ched Evans aliyehukumiwa kwa kosa la ubakaji kutumia vifaa vyao vya mazoezi. Klabu hiyo imekuwa ikishutumiwa vikali kwa kumruhusu Evans kufanya mazoezi katika klabu hiyo baada ya kuachiwa kutoka jela. Mwanariadha bingwa wa olimpiki Jessica Ennis-Hill alieleza kuwa anataka jina lake kuondolewa katika upande mmoja wa jukwaa la klabu hiyo kama mchezaji huyo angeruhusiwa kuitumikia klabu hiyop tena. Katika taarifa yake klabu hiyo imedai kuwa kutokana na malalamiko kutoka kwa mashabiki na wadau mbalimbali imeazimia kusitisha ofa yake ya kumruhusu mchezaji huyo kufanya mazoezi tena na timu hiyo. Evans aliachiwa huru mwezi uliopita baada ya kutumikia nusu ya kifungo chake cha miaka mitano jela alichohukumiwa kwa kumbakla msichana mwenye umri wa miaka 19 katika chumba cha hoteli mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment