Friday, November 21, 2014

VAN GAAL AMFAGILIA WELBECK.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Louis van Gaal amesisitiza anafurahi kumuona Danny Welbeck akipata nafasi ya kucheza mara kwa mara katika klabu ya Arsenal kwasababu asingeweza kupata nafasi hiyo katika kikosi chake. Welbeck ameanza vyema maisha mapya Arsenal baada ya usajili wa dakika za mwisho kutoka Old Trafford majira ya kiangazi ambapo mpaka sasa ameshafunga mabao matano katika mechi 12 za mashindano yote aliyocheza huku akifunga mengine matano katika mechi za Uingereza. Van Gaal amesisitiza kuwa ameshangazwa na kiwango cha nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 na anaamini maendeleo yake yametokana na kupata nafasi ya kucheza kila wiki jambo ambalo asingeweza kumuhakikishia katika kikosi chake kutokana na uwepo wa Robin van Persie, Wayne Rooney na Radamel Falcao. Kocha huyo amesema angeweza kuendelea kuitumikia United lakini waliamua kuwa anaweza kuondoka na amenufaika kwa uamuzi huo. Van Gaal amesema mchezaji yeyote anayepata nafasi ya kucheza katika timu siku huwa anaimarika na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Welbeck.

No comments:

Post a Comment