Thursday, November 20, 2014

MICHUANO YA AFCON YAIVA BAADA YA TIMU 15 ZITAKAZOSHIRIKI KUJULIKANA.

MICHEZO ya makundi ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwakani ilimalizika jana usiku huku timu tano zaidi zikifuzu huku tukishuhudia mabingwa watetezi wa michuano hiyo Nigeria wakiaga mapema. Katika michezo ya jana, Guinea moja ya nchi iliyoathirika sana na ugonjwa wa Ebola, Ivory Coast, Mali, Ghana na DR Congo zilifanikiwa kufuzu moja kwa moja na kuungana na nchi za Algeria, Burkina faso, Cameroon, Cape Verde, Congo Brazzaville, Gabon, Senegal, Afrika Kusini, Tunisia na Zambia. Mabingwa watetezi Nigeria wao walishindwa kufuzu baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Afrika Kusini ambao walikuwa tayari wamefuzu hivyo kuwafanya kumaliza katika nafasi ya tatu katika kundi A. Nafasi ya mwisho ya kufuzu ilinyakuliwa na DR Congo wakiwa kama washindi watatu bora huku Equatorial Guinea wao wakipata nafasi ya moja kwa moja kufuzu kutokana na kuwa wenyeji wa michuano hiyo. 
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Januari 17 hadi Februari na ratiba inatarajiwa kupangwa Desemba 3 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment