Thursday, November 20, 2014

MERTESACKER ABAINISHA KUMSHAWISHI OZIL KUJIUNGA NA ARSENAL.

BEKI Per Martesacker amebainisha kuwa yeye na Mesut Ozil wamezungumza na kiungo wa Real Madrid Sami Khedira kuhusu kujiunga na klabu ya Arsenal. Khedira amefanikiwa kucheza mara tano pekee tena akitokea benchi msimu huu baada ya kocha wa Madrid Carlo Ancelotti kuamua kuwatumia Toni Kroos na Luka Modric katika nafasi ya kiungo. Khedira amesisitiza hana mpango wa kuondoka Madrid pamoja na mkataba wake kukaribia kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo Mertesacker amesema ana hamu kubwa kwa Mjerumani mwenzake huyo kujiunga na Arsenal na hata kufikia hatua ya kumshawishi yeye pamoja na ozil. Octoba ilibainika kuwa Manchester United wamemtengea euro milioni 13 Khedira katik dirisha dogo la usajili Januari mwakani baada ya kuambiwa na AS Roma kuwa Kevin Strootman hatauzwa.

No comments:

Post a Comment