Thursday, November 20, 2014

BUFFON SASA KUZEEKEA JUVENTUS.

GOLIKIPA mkongwe wa Juventus, Gianluigi Buffon amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu ambao utamuweka katika klabu hiyo mpaka katika umri wa miaka 39. Buffon mwenye umri wa miaka 36 alibuka katika Serie A akiwa na klabu ya Parma mwaka 1995 na amecheza mechi 400 akiwa na Juventus toka mwaka 2001. Mkataba huo mpya wa Buffon unatarajiwa kumalizika mwaka 2017. Akihojiwa Buffon amesema anataka kuendelea kucheza katika kiwango cha juu kuisifu klabu hiyo kwani imemfanya ajivunie uamuzi wake aliofanya miaka 14 iliyopita. Mbali na Buffon Juventus pia imempa mkataba mpya beki wake wa kati Giorgio Chiellini mwenye umri wa miaka 30 ambao utamalizika mwaka 2018.

No comments:

Post a Comment