Thursday, November 20, 2014

KOCHA WA MISRI AOMBA RADHI KWA KUSHINDWA KUFUZU.

KOCHA wa timu ya taifa ya Misri, Shawky Gharib ameomba radhi kwa kushindwa kuiwezesha nchi hiyo kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwakani. Misri walishindwa kushinda mchezo wao mwisho wa makundi dhidi ya Tunisia kwa kukubalia kkichapo cha mabao 2-1. Akihojiwa mara baada ya mchezo Gharib aliwaomba radhi mashabiki wa soka wa Misri kwa kushindwa kutimiza ndoto zao. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa hajali uamuzi wowote utakaochukuliwa na Chama cha Soka cha nchi hiyo kama abaki au aondoke kwani takakubaliana nao yeye pamoja na benchi lake la ufundi. Gharib amesema alijaribu kutengeneza kikosi kipya lakini majeruhi wengi waliwakwamisha kuonyesha ubora wao. Gharib alichukua mikoba ya kuinoa nchi hiyo mwaka jana baada ya Bob Bradley kushindwa kuiwezesha timu hiyo kufuzu Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment