Thursday, November 27, 2014

EVERTON KUMUACHA ATSU.

KLABU ya Everton inafikiria uwezekano wa kumrejesha winga wa kimataifa wa Ghana Christian Atsu katika klabu yake ya Chelsea katika kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwakani. Klabu hiyo ilipambana vikali kuhakikisha inampata winga huyo kwa mkopo katika majira ya kiangazi lakini ameshindwa kung’aa Goodison Park hivyo kuifanya timu hiyo kufikiria kumuachia. Atsu mwenye umri wa miaka 22 amefanikiwa kuanza katika mechi moja pekee katika Ligi Kuu toka ajiunge na Everton. Kuna taarifa kwamba Everton imeshaanza kutafuta mbadala wa Atsu kwa kutaka kumsajili Shaun Maloney kutoka klabu ya Wigan Athletic.

No comments:

Post a Comment