Monday, November 24, 2014

RATIBA YA COPA AMERICA MWAKANI KUJULIKANA.

RATIBA ya michuano ya Copa America inatarajiwa kupangwa baadae leo huku nyota wa Barcelona Lionel Messi na Neymar wakiwa miongoni mwa wachezaji wanatarajiwa kushiriki michuano hiyo itakayofanyika majira ya kiangazi mwakani nchini Chile. Wenyeji Chile ni mojawapo mwa nchi tatu zitakazoongoza upangaji wa ratiba hiyo wakiwa sambamba na Brazil pamoja na washindi wa pili katika Kombe la Dunia Argentina. Timu 12 zinatarajiwa kukwaana katika michuano hiyo ya Amerika Kusini zikiwemo nchi zilizolikwa ambazo ni Mexico, Jamaica na mabingwa watetezi Uruguay. Hata hivyo mabingwa hao watetezi watamkosa mshambuliaji wao nyota Luis Suarez katika michuano hiyo kutokana na kuendelea kutumikia adhabu yake ya kufungiwa mechi tisa za kimataifa kwa kosa la kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika Kombe la Dunia nchini Brazil. Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi rasmi jijini Santiago Juni 11 mwakani.

No comments:

Post a Comment