Thursday, November 27, 2014

WENGER AWAKATA VILIMILIMI WANAOMKOSOA.

KLABU ya Arsenal jana imefanikiwa kuitandika Borussia Dortmund na kufuzu hatua ya mtoano ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mabao yaliyofungwa na Yaya Sanogo katika ya pili ya mchezo na Alexis Senchez katika dakika ya 57 yalitosha kuihakikishia Arsenal ushindi katika uwanja wake wa Emirates. Arsenal sasa wamejiunga Dortmund ambayo walikuwa tayari wamefuzu kutoka kundi D jana usiku ambapo pia tulishuhudia Atletico Madrid na Bayer Leverkusen nao wakifuzu hatua hiyo. Kwa upande wa Liverpool wao wana kibarua kigumu cha kujihakikishia nafasi yao katika mchezo wa mwisho dhidi ya FC Basel Uswis baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Ludogorets ya Bulgaria. Real Madrid ndio timu pekee katika michuano hiyo ambayo haijapoteza mchezo kwa kujikusanyia jumla ya alama 15 baada ya kuifunga Basle kwa bao 1-0 jana lililofungwa na Cristiano Ronaldo. Barcelona, Bayern Munich, Paris saint-Germain, Chelsea, Porto na Shakhtar Donetsk ndio timu zingine zilizofuzu kutoka katika kundi E na H hivyo kuacha nafasi tano wazi kabla ya mechi za mwisho za makundi zitakazofanyika Desemba 9 na 10 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment