Wednesday, November 26, 2014

CAF NA ADIDAS ZAZINDUA MPYA MAHSUSI WA MARHABA KWA AJILI YA MICHUANO YA AFCON MWAKANI.

SHIRIKISHO la Soka la Afrika-CAF na kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas wametoa mpira wa Marhaba kuwa maalumu kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta mwakani. Mpira huo unatarajiwa kutambulishwa rasmi Desemba 3 mwaka huu katika shughuli za upangaji ratiba za michuano hiyo ambazo zitakazofanyika jijini Malabo. Mpira huo umebuniwa kwa rangi za aina mbalimbali ambazo zinawakilisha uwanda mpana wa bara la Afrika kuanzia jangwa la sahara, rangi ya ang’avu ya samawati katika anga la bahari ya Hindi na Atlantic. Mpira huo wa Marhaba umefanyiwa vipimo vyote stahiki na kuthibitishwa kuwa unaweza kutumika katika hali yeyote katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment