Wednesday, November 26, 2014

BAYERN KUMUACHA SHAQIRI.

RAIS wa heshima wa klabu ya Bayern Munich, Franz Beckenbauer amedokeza kuwa timu hiyo inaweza kumuacha Xherdan Shaqiri katika dirisha dogo la usajili Januari mwakani. Shaqiri mwenye umri wa miaka 23 ameanza katika mechi tatu pekee za Bundesliga msimu huu huku akitokea benchi katika mechi nne za Ligi ya Mabingwa Ulaya alizocheza. Nyota huyo wa kimataifa wa Switzerland ameendelea kukosa muda wa kucheza hatua ambayo imezusha tetesi juu ya mustakabali wake na Beckernbauer anategemea Shaqiri kutafuta klabu mpya pindi dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa. Beckenbauer mwenye umri wa miaka 69 amesema Bayern tayari wameshaonyesha dalili za kutohitaji huduma ya mchezaji huyo hivyo anadhani anaweza kuondoka katika mapumziko ya majira ya baridi.

No comments:

Post a Comment