Wednesday, November 26, 2014

BARCELONA, MADRID, BAYERN WATAWALA ORODHA YA MABEKI WA FIFPro WORLD XI 2014.

KLABU za Barcelona, Real Madrid na Bayern Munich zimetawala orodha ya mabeki wateule katika kikosi cha dunia cha FIFPro World XI 2014, baada majina 12 ya wachezaji wao kuingia katika orodha kati ya majina 20 yaliyoteuliwa. Wachezaji wote wanne walioshinda nafasi ya kuwemo katika kikosi hicho mwaka jana wamejumuishwa wakiwemo Dani Alves, Philipp Lahm, Sergio Ramos na Thiago Silva. Leighton Baines, Ashley Cole, Dante na Nemanja Vidic ndio ambayo hayamo katika orodha hiyo ukilinganisha na ya mwaka jana. Kwa upande wa Madrid wamo Dani Carvajal, Pepe, Ramos, Raphael Varane na Marcelo wakati Barcelona wamo Jordi Alba, Alves, Javier Marscherano na Gerard Pique huku Bayern wakiwa na David Alaba, Lahm na Jerome Boateng. Mabeki wengine wnakamilisha orodha hiyo ni pamoja na David Luiz na Thiago Silva wa Paris Saint-Germain, Pablo Zabaleta na Vincent Kompany wa Manchester City, Branislav Ivanovic na Filipe Luis wa Chelsea, Diego Godin wa Atletico Madrid na Mats Hummels wa Borussia Dortmund. Majina manne ya washindi wa beki bora wa dunia yataamuliwa kwa kupiga kura miongoni mwa wachezaji ambapo zaidi ya wachezaji wa kulipwa 20,000 wanatarajiwa kushiriki zoezi hilo.

No comments:

Post a Comment