Wednesday, November 26, 2014

MADRID VS BARCELONA NDIO MECHI GHALI ZAIDI DUNIANI.

GAZETI moja la michezo limetoa orodha ya mechi ambazo timu zilichezesha wachezaji ghali zaidi kutokana na ada walizosajiliwa. Gazeti hilo la CIES limekuwa likiangazia ligi tano kubwa duniani katika kutoa orodha hiyo toka mwaka 2009. Mechi ya Real Madrid na Barcelona ndio ambayo imeongoza kwa kuchezesha wachezaji wengi ghali ambapo kwa ujumla wake wachezaji waliocheza walikuwa na thamani ya euro milioni 690. Katika mechi zingine zilizokutanisha wachezaji ghali ni Manchester City na Chelsea ambao kwa pamoja walikuwa na wachezaji wenye thamani ya euro milioni 578, wakifuatiwa na Paris Saint-Germain na Marseille euro milioni 503. Mechi zingine ni Bayern Munich na Borussia Dortmund euro milioni 272 na Inter Milan na Napoli euro milioni 263.

No comments:

Post a Comment