Wednesday, November 26, 2014

MENEJA WA ROMA AJIPA MOYO BAADA YA SARE DHIDI YA CSKA.

MENEJA wa klabu ya AS Roma, Rudi Garcia amesema kikosi chake kilifanya kazi ya kutosha kuhakikisha wanapata na ushindi katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya CSKA Moscow jana. Bao la kusawazisha lililofungwa na Vasili Berezutski alilofunga dakika za majeruhi lilitosha kufanya timu hizo kugawana alama kwa kufungana bao 1-1 hivyo kuweka hai matumaini yao ya kusonga mbele katika mechi zao mwisho za makundi. Garcia amesema alikuwa amefikiria tayari wameshinda mchezo huo lakini wakajikuta wakiruhusu bao katika sekunde 15 za mwisho. Huku Bayern Munich wakiwa tayari wameshatinga hatua ya timu mtoano, Roma wako katika nafasi nzuri ya kuungana nao wakijua kuwa ushindi dhidi ya Manchester City nyumbani utatosha kuwawezesha kufuzu.

No comments:

Post a Comment