Wednesday, November 26, 2014

BERAHINO AKAMATWA AKIENDESHA AKIWA AMELEWA.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya West Bromwich Albion Saido Berahino anatarajiwa kuhojiwa baada ya kukamatwa akiendesha gari huku amelewa. Mchezaji huyo mzaliwa wa Burundi mwenye umri wa miaka 21 alikamatwa kwa kuendesha mwendo kasi huko Lymm, Cheshire. Berahino alifunga bao katika sare ya mabao 2-2 iliyopata Southampton dhidi ya Manchester United. Nyota huyo anatarajiwa kurejea tena kituo cha polisi cha Cheshire kwa mahojiano zaidi Desemba baada ya kuachiwa kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment