Wednesday, November 26, 2014

ZIAYA FITI KUCHEZA KLABU BINGWA YA DUNIA - SETIF.

MABINGWA wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, ES Setif wametangaza kuwa mshambuliaji Abdelmalek Ziaya anatarajiwa kuwa fiti kwa ajili ya kushiriki michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia. Ziaya alipata majeruhi wakati wa mchezo wa fainali ya michuano hiyo dhidi ya AS Vita ya DR Congo mapema mwezi huu. Katika taarifa yake Setif walithibitisha nyota wao huyo kuanza mazoezi jana na kwamba yuko fiti kwa ajili ya mechi za mashindano. Michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mapema mwakani nchini Morocco.

No comments:

Post a Comment