Wednesday, November 26, 2014

WEZI WAMKOMBA KILA KITU WANYAMA.

MAOFISA wa polisi nchini Uingereza wanachunguza tukio la wizi lililomtokea mchezaji wa klabu ya Southampton Victor Wanyama. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Kenya aliibiwa nyumbani vitu kadhaa vikiwemo fulana ya kiungo wa Barcelona Lionel Messi, nguo za wanamitindo mbalimbali na jozi 20 za viatu. Mbali na hivyo pia aliibiwa gari lake la kifahari aina ya Land Rover lenye thamani ya shilingi milioni 8.4 kwa fedha za Kenya, fanicha, luninga pamoja na vifaa vingine vya kielektroniki. Polisi wanashangazwa na hatua kwamba majirahi wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 hawakusikia kelele zozote za uvunjaji huo.

No comments:

Post a Comment