Wednesday, November 26, 2014

KOMPANY AMMWAGIA MISIFA AGUERO BAADA YA KUIOKOA CITY.

NAHODHA wa klabu ya Manchester City, Vincent Kompany amesema Sergio Agueri ni mchezaji wa kipekee ambaye anaweza kufanya jambo lisilowezekana likawezekana. Aguero mwenye umri wa miaka 26 alifunga mabao matatu yaliyoihakikishia ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Bayern Munich waliocheza pungufu ya mtu mmoja jana na kufufua matumaini yao ya kusonga mbele katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Kompany amesema Aguaero anafanya vitu visivyowezekana vifanikiwe na hilo ni jambo muhimu kwa mchezaji wa kiwango chake. Mbali na Kompany naye meneja wa timu Manuel Pellegrini amesema nyota huyo wa kimataifa wa Argentina ni mmoja kati ya wachezaji bora kabisa duniani. City wanaweza kufuzu hatua ya timu 16 bora ya michuano hiyo kama wakifanikiwa kuitandika AS Roma katika mchezo wa mwisho wa kundi E na CSKA Moscow ikishindwa kuifunga Bayern.

No comments:

Post a Comment