Monday, December 22, 2014

ALAMA TATU ALIZOCHUKUA KWA STOKE ZAMPA JEURI MOURINHO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anaamini ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Stoke City na kuwahakikishia nafasi ya kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu katika kipindi cha Krismasi, ulikuwa na thamani zaidi ya alama tatu walizopata.Mabao ya John Terry na Cesc Fabregas walitosha kuihakikishia ushindi Chelsea na kuwafanya kuongeza pengo la alama tatu dhidi  ya wapinzani wao Manchester City. Baada ya kupata kichapo katika Uwanja wa Britannia msimu uliopita, Mourinho amefurahi msimu huu kupata ushindi katika uwanja huo. Akihojiwa Mourinho amesema kupata ushindi katika uwanja wa Stoke unatakiwa kuwa na timu nzuri yenye uwezo wa kuiga aina ya mchezo wa timu hiyo. Kocha huyo aliongeza kuwa katika kipindi hiki cha krismasi mpaka mwaka mpya wana ratiba ngumu hivyo ushindi huo ulikuwa muhimu kwao ili kuongeza morali katika timu hususani baada ya kufungwa na Newcastle United katika mchezo wao uliopita. Chelsea inakabiliwa na mchezo dhidi ya West Ham United utakaochezwa siku moja baada ya krismasi, baadae watasafiri kuifuata Southampton Desemba 28 kabla ya kuikaribisha Tottenham Hotspurs Januari mosi.

No comments:

Post a Comment