Monday, December 22, 2014

2014 KAMWE HAITASAHAULIKA KWA MADRID - ANCELOTTI.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema kitendo cha timu yake kushinda taji la Klabu Bingwa ya Dunia kinawafanya kumaliza mwaka 2014 kwa mafanikio. Mabingwa hao wa Ulaya walifanikiwa kuwafunga mabingwa wa Amerika Kusini San Lorenzo kwa mabao 2-0 na kutwaa taji hilo huko Marakech, Morocco hivyo kufikisha mataji manne kwa mwaka huu. Makombe mengine ambao yamechukuliwa na Madrid kwa mwaka huu ni pamoja na lile la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Kombe la Mfalme na Super Cup ya Ulaya. Akihojiwa Ancelotti amesema wamefanya vizuri na kamwe hawatausahau mwaka huu kwani umoja ndani ya timu umekuwa kama familia. Madrid imefanikiwa kufunga jumla ya magoli 178 kwenye mashindano yote na kuweka rekodi ya kufunga mabao mengi kwenye mwaka mmoja.


No comments:

Post a Comment