Monday, December 22, 2014

WAAMUZI 18 KUTOKA TANZANIA WATAMBULIKA FIFA.

SHIRIKISHO la soka Duniani-FIFA limetoa orodha mpya ya waamuzi linaowatambua ambapo katika orodha hiyo kuna jumla ya waamuzi 18 kutoka Tanzania, miongoni mwao wakiwemo 11 wapya na saba wa zamani. Waamuzi wapya wa kati kutoka Tanzania ni Mfaume Ali Nassor kutoka Zanzibar pamoja na Martin Saanya kutoka Morogoro, pia wamo waamuzi watatu wa kike ambao ni Florentina Zabron, Jonesia Rukyaa pamoja na Sofia Ismail. Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wanaume ni Frank John Komba na Soud Idd Lila, kwa upande wa wanawake ni Kudura Omary Maurice, Hellen Joseph Mduma, Dalila Jafari Mtwana na Grace Mawala. Waamuzi wa zamani wa Tanzania kwenye orodha ya FIFA, kwa upande wa wanaume ni Israel Mujuni Nkongo na Waziri Sheha Waziri, kwa upande wa waamuzi wasaidizi ni Josephat Bulali, Fernand Chacha, John Longino Kanyenye, Ali Kinduli na Samuel Hudson Mpenzu.

No comments:

Post a Comment