Monday, December 22, 2014

GUITERREZ KUREJEA TENA UWANJANI BAADA YA UPASUAJI WA SARATANI.

KIUNGO wa klabu ya Newcastle, Jonas Gutierrez anatarajiwa kurejea tena uwanjani akianzia mchezo wa vijana chini ya umri wa miaka 21 dhidi ya West Ham United utakaochezwa leo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 alirejea katika klabu yake hiyo mwezi uliopita na amekuwa akifanya mazoezi baada ya kufanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe wa saratani korodani. Gutierrez alifanyiwa upasuaji nchini kwao Argentina kuondoa uvimbe huo Septemba mwaka huu na baadae kupatiwa matibabu ya mionzi. Mechi yake ya mwisho kucheza ilikuwa April mwaka huu wakati Norwich City alipopelekwa kwa mkopo.

No comments:

Post a Comment