Monday, December 22, 2014

MKONGWE CAHILL BADO ATAMANI KUCHEZA KWA MIAKA MINNE ZAIDI.

MSHAMBULIAJI mkongwe wa kimataifa wa Australia, Tim Cahill anadhani kwasasa yuko fiti na anafikiri anaweza kuendelea kucheza kwa msimu minne zaidi mpaka kufikia miaka 40. Cahill amesema anatarajia kutafuta mkataba wa miaka miwili au mitatu wakati mkataba wake na klabu ya New York Red Bulls ya Marekani utakapomalizika mwakani. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 35 ambaye yuko katika kikosi cha Australia kinachojiandaa kwa ajili ya michuano ya Kombe la Asia mwezi ujao, amesema anafikiria kurejea Ligi Kuu Uingereza ambako amecheza kwa miaka tisa akiwa na Everton. Cahill amesema kwasasa bado ana mkataba na Red Bulls lakini pindi utakapomalizika anafikiria kutafuta klabu itakayompa mkataba mrefu ili aweze kuendelea kusakata kabumbu.

No comments:

Post a Comment