Tuesday, December 23, 2014

CAGLIARI YAMTIMUA KOCHA WAKE.

KLABU ya Cagliari inayoshiriki Ligi Kuu nchini Italia imemtimua kocha wake Zdenek Zeman kutokana na matokeo yasiyo ya kuridhisha kwa timu hiyo. Klabu hiyo imeshinda mechi mbili pekee chini ya kocha huyo raia wa Jamhuri ya Czech na kuwaacha katika nafasi ya 18 katika msimamo wa Serie A. Kipigo cha mabao 3-1 walichopata ugenini dhidi ya vinara wa Serie A Juventus Alhamisi iliyopita ndio ulikuwa mchezo wa mwisho kwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 67. Katika taarifa yake klabu hiyo ilimshukuru kocha huyo kwa kipindi chote ambacho wamekuwa naye kwa miezi kadhaa na kumtakia kila la heri popote atakapokwenda. Kocha wa zamani wa klabu ya Al Jazira, Walter Zenga ambaye kwasasa hana kibarua ndio anapewa nafasi ya kubwa ya kuchukua mikoba ya Zeman.

No comments:

Post a Comment