Tuesday, December 23, 2014

MOYES AMUWINDA PIENAAR.

TAARIFA kutoka nchini Uingereza zimemhusisha Steven Pienaar na tetesi za kuhamia La Liga kuungana na meneja wake wa zamani David Moyes katika klabu ya Real Sociedad. Pienaar anajulikana kwa kupendwa na Moyes kutokana na bidii zake na Everton wanaoenekana kuwa tayari kupokea ofa kwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 32. Everton wanaangalia uwezekano wa kumsajili Joel Campbell kutoka Arsenal na kama dili hilo lilikubali Pienaar anaweza kuruhusiwa kuondoka. Huu ni msimu wa nne kwa Pienaar toka ajiunge na Everton mwaka 2007 lakini majeruhi yamekuwa yakimkwamisha nyota huyo mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment