Tuesday, December 23, 2014

NILIFANYA UAMUZI SAHIHI KUJA MADRID - KROOS.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Kombe la Dunia, Toni Kroos anaamini ushindi wa Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia unaonyesha jinsi kati alivyokuwa sahihi kuondoka Bayern Munich na kwenda Real Madrid. Kiungo huyo alijiunga na Madrid katika kipindi cha majira ya kiangazi kwa kitita cha euro milioni 30 na kuisaidia timu hiyo kushinda taji hilo Jumamosi iliyopita. Madrid waliwatandika mabingwa wa soka Amerika Kusini San Lorenzo kwa mabao 2-0 katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo uliofanyika jijini Marakech, Morocco. Kroos ambaye pia alishinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia wakati akiwa Bayern amesema amefurahishwa kumaliza mwaka kwa kunyakuwa taji.  Nyota huyo amesema amefurahi kushinda taji hilo kwa mara ya pili huku akidai litakuwa na maana kubwa kwa kampeni zao za msimu huu.

No comments:

Post a Comment