Tuesday, December 23, 2014

CARRICK MCHEZAJI BORA KWA UINGEREZA KWASASA - FERGUSON.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema Michael Carrick ndiiye mchezaji bora kwa Uingereza kwasasa. Kikosi cha United kilicho chini ya Louis van Gaal kimeshinda mechi sita mfululizo toka carrick mwenye umri wa miaka 33 arejee kutoka katika majeruhi ya kifundo cha mguu Novemba mwaka huu. Akihojiwa Ferguson amesema anadhani Carrick ndio kiungo bora wa kati katika soka la Uingereza na mchezaji bora raia wa Uingereza. Kurejea kwake kumeongeza nguvu katika kikosi cha Van Gaal huku kocha huyo akimpa unahodha msaidizi Ijumaa iliyopita.

No comments:

Post a Comment