Tuesday, December 23, 2014

NAPOLI YAMALIZA UTAWALA WA JUVENTUS KWA KUNYAKUWA SUPER CUP.

KLABU ya Napoli jana ilimaliza utawala wa Juventus katika Super Cup ya Italia baada ya kufanikiwa kuifunga kwa changamoto ya mikwaju ya penati katika mchezo uliofanyika huko Doha, Qatar. Golikipa wa Napoli, Rafael ndio alikuwa nyota wa mchezo huo baada ya kuokoa penati ya Simeone Padoin. Katika muda wa kawaida Carlos Tevez aliipa Juventus bao la kuongoza kabla ya kusawazishwa na Gonzalo Higuain na kufanya timu hizo kwenda sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida na ule wa nyongeza. Ushindi unakuwa kama kisasi kwa Napoli ambao walitandikwa mabao 4-2 katika muda wa nyongeza wakati walipokutana katika mchuano huo mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment