Saturday, December 27, 2014

DI MARIA PANCHA TENA.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Manchester United, Angel Di Maria aliachwa katika mchezo ambao timu hiyo ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Newcastle United kutokana na majeruhi. Meneja wa United Louis van Gaal amebainisha Di Maria alipata majeruhi wakati wa muda wa mazoezi katika kipindi cha krismas. Kocha huyo ambaye kikosi chake kitakwaana na Tottenham Hotspurs kesho bado hajajua ni wakati gani nyota wake huyo atarejea uwanjani. Van Gaal amesema kwasasa itabidi wasubiri kuona vipimo vitakavyokuwa ili wajue ni muda gani atakaa nje. Di Maria mwenye umri wa miaka 26 ndio kwanza alikuwa amerejea katika kikosi cha United katika mchezo dhidi ya Aston Villa Desemba 20 baada ya kukosekana kwa wiki tatu kutokana na matatizo ya msuli wa paja.

No comments:

Post a Comment