Sunday, December 28, 2014

MOURINHO ALIA NA MWMAUZI KUFUATIA KUAMBULIA SARE.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anaamini kuwa kuna kampeni zinendelea kuwashawishi waamuzi kutoa uamuzi tofauti dhidi ya timu yake. Mourinho amekasirishwa na mwamuzi Anthony Taylor kwa kushindwa kutoa penati katika sare ya bao 1-1 waliyopata dhidi ya Southampton. Kiungo Cesc Fabregas alipewa kadi kwa kujirusha baada ya kuanguka katika eneo la hatari baada ya kukwatuliwa na Matt Target. Baada ya mchezo huo Mourinho aliiambia BBC kuwa vyombo vya habari, watangazaji mameneja wa timu zingine wote wanatoa shinikizo kwa waamuzi hivyo anadhani kuna kampeni inaoendelea dhidi ya timu yake. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kila anajua kuwa ni penati lakini mwamuzi alifanya makosa tena makosa makubwa pamoja na kwamba ni binadamu.

No comments:

Post a Comment