Wednesday, December 24, 2014

EFA KUAJIRI KOCHA WA KIGENI.

CHAMA cha Soka cha Misri-EFA kimetangaza kuwa kocha wake ajaye kwa ajili ya timu ya taifa ya nchi hiyo atakuwa raia wa kigeni. EFA ilimtimua kocha wa zamani, Shawky Gharib baada ya kushindwa kuipeleka nchi hiyo katika michuano ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika mwezi ujao huko Guinea ya Ikweta. Makamu wa rais wa EFA, Hassan Farid amesema baada ya kikao na wajumbe wa bodi wa chama hicho wameazimia kuwa kocha ajaye awe raia wa kigeni. Farid amesema mpaka sasa wana CV za makocha sita wa kigeni ambapo kamati husika itachagua kocha mmoja kati ya hao.

No comments:

Post a Comment