Wednesday, December 24, 2014

RONALDINHO ATISHIWA KUFUKUZWA MEXICO KWA UTORO.

RAIS wa klabu ya Queretaro ya Mexico ametishia kumfukuza Ronaldinho kama hatarejea kwa wakati katika timu hiyo. Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 34 ambaye amewahi kushinda Kombe la Dunia mwaka 2002 sambamba na tuzo za Ballon d’Or mwaka 2004 na 2005 hajarejea toka apewe likizo huku msimu mpya ukitarajiwa kuanza. Msimu mpya nchini humo unatarajiwa kuanza Januari 11 mwakani lakini Queretaro tayari wameshaanza maandalizi toka Desemba 8 huku wakiwa tayari wamecheza mechi kadhaa za kirafiki bila nyota huyo wa zamani wa Paris Saint-Germain, Barcelona na AC Milan. Rais wa klabu hiyo Arturo Villanueva ametishia kuwa kama Ronaldinho hataripoti mpaka kufikia wiki ijayo atakuwa hana jinsi bali kumtimua na nafasi yake kumpa mchezaji mwingine.

No comments:

Post a Comment