Wednesday, December 24, 2014

KHEDIRA ATAMANI KUONGEZA MKATABA MADRID.

KIUNGO wa kimataifa wa Ujerumani, Sami Khedira ameeleza kuwa atafurahi kuongeza mkataba wake na klabu ya Real Madrid kama wakifikia makubaliano. Khedira ambaye ambaye msimu huu amekuwa akiandamwa na majeruhi, amekuwa sio chaguo la kwanza la kocha Carlo Ancelotti kwani amekuwa akiwachagua Toni Kroos na Luka Modric badala yake. Vyombo vya habari vimekuwa vikitoa taarifa kuwa Khedira anaweza kuhamia Bayern Munich pamoja na vilabu kadhaa Uingereza ikiwemo Arsenal ambayo imeonyesha nia ya kuhitaji huduma yake. Khedira mabaye alijiunga na Madrid akitokea klabu ya VfB Stuttgart mwaka 2010 amedai kuwa kwasasa yuko fiti na anatumaini atapata muda zaidi wa kucheza. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kama wakifikia makubaliano anayohitaji atafurahi kuendelea kuitumikia Madrid kwa kipindi kingine zaidi ya June 2015 ambapo ndipo mkataba wake wa sasa unapomalizika.

No comments:

Post a Comment