Wednesday, December 24, 2014

KOCHA WA LEICESTER AKUBALI KUTUMIKIA ADHABU ALIYOPEWA.

MENEJA wa klabu ya Leicester City, Nigel Pearson amethibitisha jana kuwa hatakata rufani kufuatia adhabu ya kufungiwa mechi moja kufuatia kuwatukana mashabiki wa timu hiyo. Pearson alifungiwa mechi moja na kutozwa faini ya paundi 10,000 baada ya kukutwa na hatia ya kujibishana na mashabiki wakati wa mchezo dhidi ya Liverpool ambao walifungwa mabao 3-1 mapema mwezi huu. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 sasa atakosa kuwemo katika benchi la ufundi katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Tottenham Hotspurs Desemba 26 mwaka huu. Akihojiwa Pearson amesema haoni sababu ya kukata rufani kwani anataka suala hilo limalizike ili aweze kuendelea na masuala mengine.

No comments:

Post a Comment