Wednesday, December 24, 2014

CHELSEA HAINA UWEZO WA KUMSAJILI MESSI - MOURINHO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekiri kuwa hana uwezo wa kumsajili Lionel Messi kwasababu ya sheria kali za matumizi ya fedha za Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA. Mwezi uliopita Chelsea ilitangaza kuingiza faida iliyovunja rekodi ya paundi milioni 18.4 kwa mwaka uliomalizika June mwaka huu, ambayo ilichangiwa kwa kiasi kikubwa na kuongezeka kwa mapato na uuzwaji kwa wachezaji. Lakini kutokana na sheria za UEFA Mourinho amesisitiza kuwa hataweza kuwa na nafasi ya kumsajili Messi ambaye dau lake la kumng’oa Barcelona linakadiriwa kuwa paundi milioni 205. Akihojiwa na kituo kimoja cha redio kocha huyo Mreno amesema hawezi kuwa na nafasi hiyo kutokana na sheria za sasa za UEFA zinazoweka kikomo matumizi ya vilabu ili kujaribu kuweka usawa kwa vilabu vingine visivyokuwa na pesa.

No comments:

Post a Comment