Monday, December 29, 2014

NAFURAHI KUREJEA NYUMBANI - TORRES.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Hispania, Fernando Torres ameeleza furaha yake ya kukubali kujiunga na Atletico Madrid kwa mkopo kutoka AC Milan mpaka mwishoni mwa msimu ujao. Nyota huyo ameshindwa kung’ara akiwa na Milan baada ya kujiunga nao kwa mkopo Agosti, ambapo amefunga bao moja katika mechi 10 za Serie A alizocheza. Hata hivyo, baada kukubali kujiunga kwa mkataba wa moja kwa moja na Milan, Torres mwenye umri wa miaka 30 sasa amekubali kujiunga na Atletico kwa mkopo klabu ambayo ndio iliyomuibua akiwa kinda. Torres amesema kuna wakati kila atalazimika kurudi nyumbani ivyo anajisikia furaha kurejea tena mahali alipoibukia. Nyota huyo amesema kwa kipindi kirefu amekuwa amekuwa akisema hawezi kuficha alipotokea hivyo ni heshima kubwa kwake kurejea tena Atletico.

No comments:

Post a Comment