Monday, December 29, 2014

VAN GAAL ASINGIZIA UCHOVU WA SIKUKUU KUFUATIA SARE DHIDI YA SPURS.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Louis van Gaal amedai kuwa kikosi chake kilikuwa kikipambana kutafuta uhai katika kipindi cha pili kwenye mchezo dhidi ya Tottenham Hotspurs uliomalizika kwa sare ya bila ya kufungana. Ushindi katika mchezo huo ungewawezesha United kupunguza pengo la alama dhidi ya timu za Chelsea na Manchester City ambao wote nao walipoteza alama. Van Gaal amelaumu ratiba ngumu ya kipindi cha sikukuu kuwa chanzo kikubwa kwa kikosi chake kushindwa kufanya vyema katika mchezo wa jana. Kocha huyo amesema kisayansi imethibitishwa kuwa mwili hauwezi kurejea katika hali yake ya kawaida katika muda wa saa 48.

No comments:

Post a Comment