Monday, December 29, 2014

TOURE KUIKOSA SUNDERLAND MWAKA MPYA.

KLABU ya Manchester City inatarajiwa kukosa huduma ya kiungo wake Yaya Toure katika mchezo dhidi ya Sunderland Alhamisi hii kutokana na kusumbiliwa na matatizo ya nyonga. Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alikosa mchezo dhidi ya Burnley jana akisumbuliwa na majeruhi ya msuli aliyopata katika mchezo dhidi ya West Bromwich Albion uliochezwa Desemba 26. Huku wakiwa tayari wamewakosa Sergio Aguero, Edin Dzeko na Vincent Kompany, City watakuwa wakikabiliwa na mtihani mwingine wa kukosa Toure. Meneja wa City manuel pellegrini amebainisha kuwa ingekuwa hatari kumchezesha Toure katika mchezo dhidi ya Burnley na kuthibitisha kuwa watafuatilia afya yake inavyoendelea leo.

No comments:

Post a Comment