Monday, December 29, 2014

SANCHEZ AKANUSHA KUWA NYOTA ARSENAL.

MSHAMBULIAJI mahiri wa klabu ya Arsenal, Alexis Sanchez amekanusha taarifa kuwa yeye ndio nyota wa timu hiyo kwa msimu huu, akisisitiza yeye ni kama wachezaji wengine. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Chile alihamia Emirates kwa kitita cha euro milioni 40 wakati wa majira kiangazi na sasa anaongoza akiwa amefunga mabao 15 msimu huu. Lakini pamoja na hayo, Sanchez anaamini kuwa meneja Arsene Wenger ana vipaji vingi katika kikosi chake. Sanchez amesema hakubaliani na suala la kuwa nyota kwani kikosi chao kina wachezaji wengi wakubwa wenye hadhi ya dunia. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa katika kikosi cha Arsenal yeye ni kama wachezaji wengine, ila amepata bahati ya kuanza vyema.

No comments:

Post a Comment