Wednesday, December 24, 2014

REDKNAPP AMKOMALIA AUSTIN.

MENEJA wa klabu ya Queens Park Rangers-QPR, Harry Rednapp amesema mshambuliaji wake kinara wa mabao Charlie Austin hatauzwa katika usajili wa dirisha dogo Januari mwakani lakini mustakabali wake utategemea kubaki kwa timu hiyo katika Ligi Kuu. Austin mwenye umri wa miaka 25 ambaye amefunga mabao 11 msimu huu na kumfanya kuwa mchezaji anayeongoza kwa mabao katika ligi Uingereza amebakisha miezi 18 katika mkataba wake wa sasa. Akihojiwa na wana habari kuelekea safari yao ya kuifuata Arsenal kesho, Redknapp amesema hana mpango wa kumuuza mshambuliaji huyo katika dirisha dogo. Lakini pamoja na hayo Redknapp amekiri kuwa hataweza kumzuia katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi kama wakishindwa kubaki katika Ligi Kuu kwasababu mwenyewe anataka kuendelea kucheza hapo mpaka atakapostaafu. QPR haijapata alama yeyote ugenini msimu huu lakini alama 17 walizofanikiwa kuzichukua katika mechi zao za nyumbani zimewasaidia kuwaondoa katika hatari ya kushuka daraja mpaka nafasi ya ya 16.

No comments:

Post a Comment