Wednesday, December 24, 2014

BARCELONA KWENDA QATAR FEBRUAR KUTIMIZA MSHARTI YA MDHAMINI.

KLABU ya Barcelona, inatarajiwa kusafiri kuelekea nchini Qatar kwa ajili ya mchezo wa kirafiki Februari 4 mwakani. Barcelona ambao kwasasa wako katika nafasi ya pili ya msimamo wa La Liga wanatarajia kucheza mechi hiyo kwa ajili ya kutimiza masharti ya mdhamini wao Kampuni ya Uwekezaji ya Michezo ya Qatar wanaodhamini fulana zao. Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa Jumatano, siku tatu baada ya mchezo wa nyumbani dhidi ya Villarreal huku wakikabiliwa na mchezo mwingine dhidi ya Athletic Bilbao Februari 8. Mechi hiyo ilitangazwa wakati wa kikao cha bodi ya klabu hiyo lakini haikutajwa timu atakayocheza nayo.

No comments:

Post a Comment