Wednesday, December 24, 2014

ALEX SONG APIGWA CHINI CAMEROON.

KOCHA wa timu ya taifa ya Cameroon, Volke Finke ametaja kikosi cha awali cha wachezaji 27 kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika itakayofanyika huko Guinea ya Ikweta. Kocha huyo raia wa Ujerumani ameteua wachezaji wengi waliokuwemo katika mechi za kufuzu, lakini amemuacha kiungo Alex Song. Song hajaichezea Cameroon toka alipotolewa nje kwa kadi nyekundu katika kipindi cha mabao 4-0 walichopata kutoka kwa Croatia katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil. Kiwango kizuri alichokionyesha msimu huu akiwa kwa mkopo katika klabu ya West Ham United akitokea Barcelona, kilizua tetesi kuwa angeweza kuitwa katika timu ya taifa. Cameroon wanatarajiwa kuanza maandalizi nyumbani na watacheza mechi ya kirafiki na Congo Brazzaville Januari 7 kabla ya kusafiri kwenda Gabon kwa ajili ya kambi yao nyingine na kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini Januari 11.

No comments:

Post a Comment