Wednesday, December 24, 2014

TETESI ZA USAJILI: UNITED YAMTENGEA BALE PAUNDI MILIONI 120, ARSENAL WAJIPANGA KUCHUKUA CAVANI.

UONGOZI wa klabu ya Manchester United, umedai kuwa tayari kutoa kitita cha paundi milioni 120 kwa ajili ya kumsajili winga Gareth Bale mwenye umri wa miaka 25 kutoka klabu ya Real Madrid katika dirisha dogo la usajili Januari mwakani. Bale ambaye ni mmoja kati ya wachezaji ghali zaidi ulimwenguni alisajiliwa na Madrid kwa kitita kilichoweka rekodi cha paundi milioni 85.3 mwaka 2013. Wakati huo huo kocha Laurent Blanc wa klabu ya Paris Saint-Germain anafikiria kumuachia mshambuliaji wake Edinson Cavani mwenye umri wa miaka 27 kwa gharama ya paundi milioni 50 kama Arsenal watamhitaji katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo. Kwingineko Manchester City nao imetenga kitita cha paundi milioni 25 kwa ajili ya kumuwinda mshambuliaji wa Atletico Madrid Mario Mandzukic mwenye umri wa miaka 28.

No comments:

Post a Comment